Wednesday 28 September 2016

DC SERENGETI AIPONGEZA PSPF KWA KUTOA HUDUMA NZURI

Habari toka kitengo cha Habari na Mawasiliano HALMASHAURI YA WILAYA YA SERENGETI.


Mkuu wa wilaya ya Serengeti, Nurdin Babu ameipongeza Taasisi ya Mfuko wa Pensheni kwa watumishi wa umma kwa huduma nzuri wanazotoa kwa wateja wao.
Pongezi hizo zimetolewa katika semina iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti ambapo wataalamu kutoka PSPF walikutana na watumishi wa serikali kutoka taasisi mbali mbali ndani ya wilaya ya Serengeti.

Katika hotuba aliyotoa, Babu alisema “Taasisi ya PSPF imekuwa na mchango mkubwa kwa serikali katika kuwahudumua watumishi wa serikali kwa kutunza amana zao pamoja na kutoa mikopo inayowanufaisha wateja wake nawapongeza sana kwa huduma zenu nzuri mnazotoa” aliendelea kwa kusema “watumishi tumieni fursa zitolewazo na PSPF katika kufanya shughuli za kimaendeleo”
Akiongea kuhusu huduma wanazotoa, Meneja wa PSPF Mkoa wa Mara, Bwana Deogratius Njuu alisema “PSPF tumekuwa mstari wa mbele kuhakikisha kuwa tunatoa huduma bora kwa wateja wetu” aliongezea kwa kusema kuwa “Wateja wa PSPF wananufaika na mkopo wa kujikimu unaotolewa kwa watumishi wapya, mkopo wa kujiendeleza kielimu na pia tunatoa mikopo ya viwanja vilivyopimwa kwa ajili ya makazi”
Aidha watumishi walioudhiria semina hiyo waliipongeza PSPF kwa kuwafikia katika maeneo ya kazi na kuwaomba kuboresha mahusiano zaidi na wateja wao na kufika vijijini pia kutoa elimu hiyo. 

                                          MATUKIO KATIKA PICHA
Meneja wa PSPF Mkoa wa Mara Bw. Deogratius Njuu akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Serengeti Mhe. Nurdin Babu
















No comments:

Post a Comment