Wednesday 7 September 2016

ZIARA YA MKUU WA MKOA WA MARA WILAYANI SERENGETI


Habari toka kitengo cha Habari na Mawasiliano Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti.

 Mkuu wa wilaya ya Serengeti Nurdin Babu (Kulia) akimpokea Mkuu wa Mkoa wa Mara Dk. Charles Mlingwa




Mkuu wa Mkoa wa Mara Dk. Charles Mlingwa jana tarehe 06 Septemba 2016 amefanya ziara ya kujitambulisha katika Wilaya ya Serengeti na kukutana na watumishi wa taasisi za serikali, taasisi zisizo la serikali, viongozi wa dini, wadau wa maendeleo pamoja na waheshimiwa madiwani.



Katika kikao hicho, Mkuu wa Wilaya ya Serengeti, Nurdin Babu aliwasilisha kero kubwa mbili zinazowakabili wananchi ambazo ni Ukosefu wa Maji Safi na Salama pamoja na Uharibifu wa Mali na Mazao unaofanywa na Tembo wanaovamia vijiji hata kufikia hatua ya kuuwa wananchi.



Dk. Mlingwa akijibu, alisema kuwa “Anazitambua kero hizo na juhudi za dhati zinafanyika kutatua kero hizo kwa wananchi wa wilaya ya Serengeti” Kuhusu ukosefu wa maji safi na salama katika mji wa mugumu alisema kuwa, “ Ni mwezi wa nne (4) sasa wakazi wa mugumu hawana maji na kuiagiza idara husika kuhakikisha maji yapatikana mapema iwezekanavyo” Dk. Mlingwa ametilia mkazo suala la maendeleo na kuzitaka taasisi husika ndani ya wilaya ya Serengeti kusukuma gurudumu la maendeleo ili kuleta tija kwa Wilaya na Mkoa wa Mara kwa ujumla.



Aidha Dk. Mlingwa ameipongeza Halmshauri ya Wilaya ya Serengeti kwa kuhakikisha mji wa mugumu unapata lami huku Mkandarasi SAMOTA Construction Ltd akiwa yupo eneo la kazi akiendelea na hatua za awali ya uwekaji wa lami. Hata hivyo Dk. Mlingwa amesikitishwa na uchelewaji wa kukamilika kwa ujenzi wa barabara ya lami kutoka Butiama mpaka Mugumu Serengeti huku akitilia mashaka uwezo wa wakandarasi hao kukamilisha awamu hiyo ya kwanza ya barabara ya lami ya kilometa 50 itakayoishia Sanzati.


Dk. Mlingwa alipata muda wa kutembelea Bwawa la Machira na kuona jitihada za Halmashauri pamoja na Idara ya maji Mji wa Mugumu kurejesha hali ya upatikanaji wa maji. Ziara hiyo ya siku 3 pia itahusisha kutembelea miradi ya afya na maji ndani ya Wilaya ya Serengeti.



                        MATUKIO KATIKA PICHA
















No comments:

Post a Comment