Tuesday 31 January 2017

KITUO CHA AFYA NATTA CHAPATA GARI MAALUM LA WAGONJWA (AMBULANCE)

Habari kutoka Kitengo cha TEHAM & UHUSIANO
HALMASHAURI YA WILAYA YA SERENEGTI

Serikali Wilayani Serengeti Mkoa wa Mara yaikabidhi Kituo cha Afya Natta Gari maalumu ya kuwahisha wagonjwa (ambulance). Makabidhiano ya gari hilo yamefanyika siku ya jana tarehe 31 Januari 2017 nje ya Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti. Akikabidhi gari hilo Mkuu wa Wilaya ya Serengeti Mhe. Nurdin Babu ameitaka Idara ya afya Wilayani kuboresha upatikanaji wa huduma ya haraka ili kupunguza idadi ya vifo vitokanavyo na ukosefu wa huduma ya haraka.
Gari maalumu Kwa ajili ya kubeba wagonjwa (Ambulance) lilitoloewa na Wizara ya Afya Kwa ajili ya kuboresha huduma za matibabu katika Kituo cha afya cha Natta Wilayni Serengeti.




Mkuu wa Wilaya ya Serengeti, Mhe. Nurdin Babu (katikati) akikabidhi kati ya gari kwa Diwani wa Kata ya Natta Mhe. Juma Porini Keya (kushoto) 

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti ambae pia ni Diwani wa Kata ya Natta, Mhe Juma Porini Keya akishukuru Wizara ya afya kwa kufanikisha upatikanaji wa Gari hilo

DC Nurdin Babu akijaribu kuwasha gari hilo.