Sunday 4 September 2016

HARAMBEE YA UKAMILISHAJI UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI ROBANDA TAREHE 2 SEPTEMBA 2016



Mkuu wa Wilaya ya Serengeti Mhe. Nurdin Babu (kushoto) akisalimiana na Mgeni Rasmi wa Harambee hiyo Mhifadhi Mkuu Hifadhi ya Taifa ya Serengeti Bw. William Mwakilema.

Harambee ya ukamilishaji wa ujenzi wa Shule ya Sekondari Robanda iliyofanyika katika majengo ya shule hiyo iliyopo katika kijiji cha Robanda imefanikiwa kupata jumla ya fedha taslimu Tsh Milioni 11,299,000 na fedha za kigeni 13 US Dollars zilipatikana papo hapo pamoja na ahadi ya fedha kiasi cha Tshs Mil 42,499,500 fedha za kigeni 2,000 US Dollars, Mifugo Ng'ombe watano (5), mbuzi wawili (2). Serikali ya kijiji cha Robanda imeahidi kujenga nyumba moja (1) ya kuishi walimu huku Kampuni ya Thomson Safari ikiahidi kujenga nyumba tatu za kuishi walimu na kuwa na jumla ya nyumba nne (4) zote zikiwa na thamani ya Tshs Milioni 290. Mifuko ya Saruji 237 iliahidiwa kukamilisha ujenzi wa shule hiyo kutoka kwa wadau mbali mbali wa maendeleo walioshiriki harambe hiyo. Aidha Benki ya Posta tawi la Musoma imechangia madawati 50, huku wadau wengine wa maendeleo kuongezea madawati manne (4) na kufanya idadi ya madawati yaliyochangiwa kufikia 54. Akitoa shukrani za dhati Mgeni rasmi katika harambee hiyo Mhifadhi Mkuu toka HIfadhi ya Taifa ya Mbuga ya Wanyama Serengeti Bw William Mwakilema alisema “anashukuru wale wote walioguswa na kuchangia ujenzi wa shule hiyo kwani kukamilika kwake kutasaidia wanafunzi waishio maeneo jirani na robanda kuwa na shule karibu na kuondoa adha ya umbali mrefu wanaotumia wanafunzi hao kwenda shuleni”
Harambe hiyo iliudhuliwa na Mkuu wa Wilaya ya serengeti Mhe. Nurdin Babu, Katibu Tawala Wilaya ya Serengeti Bw. Cosmas Quamara na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti Bw. Juma Hamsini Seph pamoja na Waheshimiwa Madiwani pia walijitokeza kuunga mkono Mhe. Diwani wa Kata ya Ikoma Mhe. Michael Kunani huku wageni kutoka ndani na nje ya wilaya ya serengeti walijitokeza na kufanikisha upatikanaji wa michango hiyo. Mpaka sasa shule hiyo bado haijaanza kupokea wanafunzi kutokana kutokamilika kwa baadhi ya majengo zikiwemo nyumba za walimu. kukamilika kwa majengo na uwekaji wa thamani kutaboshera hali ya elimu katika kata ya Ikoma.

                            MATUKIO KATIKA PICHA 
Mhe Diwani Kata ya Ikoma Bw. Michael Kunani (kushoto) akimkaribisha Mkuu wa Wilaya Serengeti Mhe. Nurdin Babu (kati kati) kushoto ni Afisa Tarafa wa Grumet Bw, Paul Shanyangi
Mhe Diwani Kata ya Ikoma (kushoto) akimkaribisha Mgeni Rasmi wa Harambee (kulia) Mhifadhi Mkuu SENAPA Bw. William Mwakilema


Wadau wa maendeleo walijitokeza kwa wingi na kuchangia maendeleo kata ya Ikoma




Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti Bw. Juma Hamsini Seph

Katibu Tawala Wilaya ya Serengeti Bw. Cosmas Quamara

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti/ Diwani wa Kata ya Natta Mhe. Juma Porini Keya


Jumla ya Tsh Mil 11,299,000  zilichangwa papo hapo.

1 comment:

  1. kazi nzur jaman...na hzo pesa zsimamiwe vzur bas ili lengo litimie...pongez kwa wadau wote wa maendeleo wilayan serengeti na wote waliofanikisha zoez hilo...

    ReplyDelete