Monday 31 October 2016

SERENGETI NA BUNDA ZANUFAIKA NA UWEKEZAJI WA SINGITA GRUMETI.

Habari toka Kitengo cha TEHAMA & MAHUSIANO
HALMASHAURI YA WILAYA YA SERENGETI.

Mfuko wa Singita Grumeti umeendelea kuwa mstari wa mbele katika kuboresha hali ya elimu katika Wilaya za Serengeti na Bunda.
Hii imedhihirika kwenye halfa ya kukabidhi madawati 500 kwa Mkuu wa Mkoa wa Mara Dk. Charles Mlingwa ili kupunguza uhaba wa madawati katika Wilaya hizo. Aidha Grumeti wamekabidhi nyumba ya kuishi mwalimu iliyojengwa katika Shule ya Msingi Makundusi.

Mkuu wa Huduma za Jamii Singta grumeti Richard Ndaskoi (kulia) akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Mara Dk. Charles Mlingwa msaada wa madawati 500 yenye Thamani ya Tshs Milioni 112 kwa ajili ya Wilaya za Serengeti na Bunda katika hafla  iliyofanyika  Shule ya Msingi Makundusi Wilayani Serengeti.
“Tuko hapa kukabidhi madawati haya 500 yenye thamani ya Tshs. Milioni 112 kwa Wilaya za Serengeti na Bunda pamoja na nyumba hii yenye thamani ya Tshs. Milioni 86” alisema Richard Ndaskoi ambae ni Mkuu wa Huduma za Jamii toka Mfuko wa Singinta Grumeti.
Akipokea misaada hiyo, Dk. Mlingwa alisema “Nawashukuru Singita Grumeti kwa Msaada huu wa madawati pamoja na nyumba hakika mchango wenu katika Mkoa wa Mara unaoneka” Dk Mlingwa amewataka wawekezaji wengine katika Mkoa wa Mara kuchangia madawati katika Wilaya za Serengeti na Bunda kwani bado zina uhaba wa madawati. 
Aidha Dk. Mlingwa ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti kwa kuwa na mahusiano mazuri na wawekezaji waliopo katika Wilaya hiyo “Tukiwawekea mazingira mazuri ya kufanya shughuli zao hata wananchi pia watanufaika na uwepo wa wawekezaji hawa” alisema Dk. Mlingwa.
Naye Mkuu wa Wilaya ya Serengeti, Nurdin Babu pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Bunda, Lydia Bupilipili wote kwa nyakati tofauti wameushukuru Mfuko wa Singita Grumeti kwa msaada huo wa madawati na kuuomba mfuko huo kuendelea kuchangia katika shughuli za maendeleo katika Wilaya za Serengeti na Bunda. “Wilaya hii ina wawekezaji wengi lakini wamekuwa nyuma katika kuchangia shughuli za maendeleo, nawapongeza kwa kuwa mstari wa mbele kusaidia jamii inayowazunguka pamoja na kuchangia katika maendeleo ya Wilaya ya Serengeti” alisema Nurdin Babu.
Aidha Bi. Bupilipili ameuomba Mfuko huo kuanzisha kampeni maalumu ya kuongeza kiwango cha ufaulu kwa watoto wa kike kwa shule za sekondari Wilayani Bunda.
Singita Grumeti wamekuwa wawekezaji wenye tija kwa wananchi wa Wilaya za Serengeti na Bunda licha ya kuwa mstari wa mbele kuchangia katika shughuli za maendeleo, kampuni hiyo pia imekuwa ikitoa ajira kwa wakazi toka wilaya hizo mbili pamoja na kutoa ufadhili wa masomo kwa wanafunzi toka wilaya hizo.
Mkurugenzi wa Singita Grumeti Stephen Cunliffe (kulia) akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Mara Dk. Charles Mlingwa msaada wa madawati 500 yenye Thamani ya Tshs Milioni 112 kwa ajili ya Wilaya za Serengeti na Bunda katika hafla  iliyofanyika  Shule ya Msingi Makundusi Wilayani Serengeti.


Mkurugenzi wa Singita Grumeti Stephen Cunliffe (kulia) akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Mara Dk. Charles Mlingwa nyumba ya kuishi mwalimu yenye thamani ya Tshs Milioni 86 iliyojengwa katika Shule ya Msingi Makundusi Wilayani Serengeti.


Thursday 20 October 2016

MAPATO YA MINADA WILAYANI SERENGETI YAONGEZEKA.

Habari toka Kitengo cha Habari na Mawasiliano.
HALMSHAURI YA WILAYA YA SERENGETI.


Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti, Mhe. Juma Porini Keya akitoa risiti kwa kutumia kifaa cha POS.

“Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti imefanikiwa kuongeza mapato yatokanayo na minada mbali mbali inayofanyika ndani ya Wilaya”

Hayo yamesemwa na Terry Hurson ambae ni Kaimu Mtunza Fedha wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti alipokuwa anazungumza na Waheshimiwa Madiwani wanaounda Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango waliofanya ziara katika Mnada wa Kijiji cha Rung’abure kilichopo Kata ya Rung’abure.

Ziara hiyo ya ukaguzi ni mwendelezo wa taratibu zilizowekwa na Serikali kwa kuwahusisha Waheshimiwa Madiwani wanaounda Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango kutembelea miradi kila baada ya miezi mitatu (Robo Mwaka wa Serikali)

Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango inayoongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti, Juma Porini Keya pamoja na Katibu wa Kamati hiyo ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti Juma Hamsini pamoja na wajumbe wa Kamati walijionea jinsi ukusanyaji wa mapato unavyofanyika kwa kutumia vifaa vya kieletroniki (POS) vinavyotumika pia kutoa risiti za malipo. “Mapato ya Minada yameongezeka kutokana na kuzuia mianya ya ukwepaji wa kodi na matumiz ya POS” alisema Terry Hurson. Aliongeza kwa kusema "kipindi cha mzabuni mapato yatokanayo na mnada wa kijiji cha Rung'abure yalikua ni Tshs Milioni 2.4 kwa mwezi na sasa tunakusanya wastani wa Tshs Milioni 3.2"

Ukusanyaji wa mapato unafanywa na watumishi wa Serikali, hii ni baada ya Serikali ya awamu ya tano ikiongozwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli kuzitaka Halmashauri zote nchini kukusanya mapato na kuacha kutumia wazabuni katika kukusanya mapato kwenye masoko na minada.

                                                             MATUKIO KATIKA PICHA
Kutoka Kushoto Mhe. Juma Porini Keya, katikati ni Bw. Terry Hurson (Kaimu Mtunza Fedha) kushoto ni Charles Ghati (Mkusanyaji wa Mapato) katika mnada wa Rung'abure.


Wafanyabiashara katika mnada wa kijiji cha Rung'abure wakifanya malipo.
Huduma za chakula pia hupatikana.


MAPATO YA MINADA WILAYANI SERENGETI YAONGEZEKA.

Habari toka Kitengo cha Habari na Mawasiliano.
HALMSHAURI YA WILAYA YA SERENGETI.


Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti, Mhe. Juma Porini Keya akitoa risiti kwa kutumia kifaa cha POS.

“Halmashauri ya wilaya ya Serengeti imefanikiwa kuongeza mapato yatokanayo na minada mbali mbali inayofanyika ndani ya Wilaya”

Hayo yamesemwa na Terry Hurson ambae ni Kaimu Mtunza Fedha wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti alipokuwa anazungumza na Waheshimiwa Madiwani wanaounda Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango waliofanya ziara katika Mnada wa Kijiji cha Rung’abure kilichopo Kata ya Rung’abure.

Ziara hiyo ya ukaguzi ni mwendelezo wa taratibu zilizowekwa na Serikali kwa kuwahusisha Waheshimiwa Madiwani wanaounda Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango kutembelea miradi kila baada ya miezi mitatu (Robo Mwaka wa Serikali)

Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango inayoongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti, Juma Porini Keya pamoja na Katibu wa Kamati hiyo ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti Juma Hamsini pamoja na wajumbe wa Kamati walijionea jinsi ukusanyaji wa mapato unavyofanyika kwa kutumia vifaa vya kieletroniki (POS) vinavyotumika pia kutoa risiti za malipo. “Mapato ya Minada yameongezeka kutokana na kuzuia mianya ya ukwepaji wa kodi na matumiz ya POS” alisema Terry Hurson.


Ukusanyaji wa mapato unafanywa na watumishi wa Serikali, hii ni baada ya Serikali ya awamu ya tano ikiongozwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli kuzitaka Halmashauri zote nchini kukusanya mapato na kuacha kutumia wazabuni katika kukusanya mapato kwenye masoko na minada.

                                                   MATUKIO KATIKA PICHA
Kutoka Kushoto Mhe. Juma Porini Keya, katikati ni Bw. Terry Hurson (Kaimu Mtunza Fedha) kushoto ni Charles Ghati (Mkusanyaji wa Mapato) katika mnada wa Rung'abure.


Wafanyabiashara katika mnada wa kijiji cha Rung'abure wakifanya malipo.
Huduma za chakula pia hupatikana.


Sunday 9 October 2016

WAWEKEZAJI WILAYANI SERENGETI WAHIMIZWA KUCHANGIA SHUGHULI ZA MAENDELEO

Habari toka Kitengo cha Habari na Mawasiliano HALMASHAURI YA WILAYA YA SERENGETI.




Serikali wilayani Serengeti imewataka wawekezaji kulipa kodi na kuchangia katika shughuli za maendeleo ndani ya Wilaya ya Serengeti.
Mkuu wa Wilaya ya Serengeti Mhe. Nurdin Babu (aliyesimama) akiongea na wadauwa maendeleo katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti.



Hayo yamejiri jana Oktoba 8 2016 katika katika kikao cha wadau wa maendeleo kilichoitishwa na Mkuu wa wilaya ya Serengeti Mheshimiwa Nurdin Babu alipokuwa akizungumza na wawekezaji waliopo wilayani Serengeti katika ukumbi wa mikutano wa Halmshauri.“Tunataka kukamilisha ujenzi wa hospitali yetu ya wilaya na nyinyi ni wadau wetu wakubwa katika maendeleo” alisema Mheshimiwa Babu. Aidha Mheshimiwa Babu amesikitishwa na kitendo cha wawekezaji waliopo katika wilaya ya Serengeti kutochangia katika shughuli za maendeleo hali kadhalika kutojitokeza kabisa kwa wahusika wakuu wa makampuni pindi wanapohitajika.
Aidha Mwenyekiti wa Halamshauri ya Wilaya ya Serengeti Mheshimiwa Juma Porini Keya amezitaka kampuni zenye kambi za utalii wilayani Serengeti kulipa kodi na tozo stahiki kwa serikali ili kuiwezesha Serikali kupitia Halmashauri kutoa huduma bora kwa wakazi wa Serengeti. Katika hatua nyingine Mheshimiwa Porini ameziomba kampuni zenye kambi za utalii katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti kuajili watu kutoka wilayani Serengeti “Naamini Serengeti wapo vijana wenye sifa za kuajiliwa katika kampuni za utalii hifadhini” alisema Mheshimiwa Porini.



Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti Bw. Juma Hamsini alimpongeza Mkuu wa Wilaya kwa juhudi anazofanya kuhakikisha ujenzi wa Hospitali ya Wilaya unakamilika na kushauri iundwe kamati itakayo wajumuisha wahifadhi pamoja na kampuni za utalii kushughulikia suala la ukamilishaji wa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Serengeti.
Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti ilianzisha mradi wa Ujenzi wa Hospitali ya Wilaya mjini Mugumu kuanzia mwaka wa bajeti 2007/2008 ili kuimarisha huduma kwa wagonjwa wanaopewa rufaa kutoka vituo 54 vya huduma ya afya vilivyopo wilayani na wale wanaotoka katika mji wa Mugumu na vijiji jirani. Aidha wazo la kujenga Hospitali hiyo liliungwa mkono na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa awamu ya nne Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete baada ya kuona umuhimu wa ujenzi wa Hospitali hii ili kutoa huduma kwa jamii na wageni wajao nchini kutembelea vivutio vya Kitalii vilivyoko jirani na Mji wa Mugumu hasa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti. Mpaka sasa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya umekwama kutokana na Halmashauri kutopata fedha kukamilisha ujenzi wa Hospitali.








   Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti Bw. Juma Hamsini
Mganga Mkuu wa Wilaya ya Serengeti Dk. Manyatta akifafanua jambo kwa wajumbe wa kikao.
Wajumbe wa Kikao walitembelea majengo ya Hospitali ambayo ujenzi umesimama, kutoka kushoto ni Dk Manyata (Mganga Mkuu wa Wilaya) katikati ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti Mhe Juma Porini Keya, Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Serengeti Mhe. Nurdin Babu.

 






Wednesday 5 October 2016

KATIBU TAWALA MKOA WA MARA AFANYA ZIARA WILAYANI SERENGETI

Habari toka Kitengo cha Habari na Mawasiliano- HALMASHAURI YA WILAYA YA SERENGETI


Katibu Tawala Mkoa wa Mara Bw. Ado Stephen Mapunda, leo tarehe 5 Oktoba 2016 amefanya ziara ya kujitambulisha katika Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti na kufanya mazungumzo na watumishi wa Halmashauri.
            Katibu Tawala Mkoa wa Mara, Bw. Ado Stephen Mapunda akizungumza na watumishi wa
                                                           Halmashauri ya wilaya ya Serengeti.
Katika kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Halmashauri, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Bw. Juma Hamsini alimpongeza  Bw. Mapunda kwa kuteuliwa na Rais John Pombe Magufuli kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara na kuahidi kufanya nae kazi kwa umoja ili kuleta maendeleo katika Wilaya ya Serengeti na Mkoa wa Mara kwa ujumla.

Mapunda alipata wasaa wa kuongea na watumishi ambapo aliwataka kufanya kazi kwa bidii licha ya kuzungukwa na mazingira magumu ya kazi pia kuwa wabunifu kwa kubuni miradi itakayowanufaisha wananchi wa Serengeti. Katibu Tawala amewataka watumishi wa umma kujiendeleza kielimu na kuongeza maarifa ili kuongeza ufanisi wa kazi wakiwa kazini “Msibweteke na elimu mlizonazo na kusahau kwenda kujiendeleza kielimu” alisema Mapunda. Aidha Mapunda amewataka watumishi wa umma kutumia vizuri kipato wanachopata kwa kujiwekea akiba na kufanya shughuli za maendeleo.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti, Mhe. Juma Porini Keya ambaye pia alihudhuria kikao hicho amempongeza Bw. Mapunda kwa uteuzi na kuahidi kutoa ushirikiano katika kuleta maendeleo kwa wananchi wa Serengeti na kuwataka watumishi wa Halmashauri kuyafanyia kazi yale yote aliyosema Katibu Tawala Mkoa wa Mara.

Tarehe 10 Septemba 2016, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli alimteua Bw. Ado Stephen Mapunda kuwa Katibu Tawala Mkoa wa Mara na kuziba nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Benedict Ole Kuyan ambaye amestaafu.

      Katibu Tawala Mkoa wa Mara (kushoto) Bw. Ado Stephen Mapunda Akiwasili katika
        Ukumbi wa Mikutano wa Halamshauri, kulia ni Katibu Tawala Wilaya ya Serengeti
 Bw. Cosmas Qamara

     Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri yaWilaya ya Serengeti Bw. Juma Hamsini (aliyesmama)
        akimkaribisha Katibu Tawala Mkoa wa Mara tayari kwa mazungumzo na watumishi.

             Sehemu ya watumishi waliojitokeza kumsikiliza Katibu Tawala Mkoa wa Mara

Tuesday 4 October 2016

NIDA WAANZA KUSAJILI NA KUHAKIKI WATUMISHI WA UMMA WILAYANI SERENGETI

Habari kutoka Kitengo cha Habari na Mawasiliano - HALMASHAURI YA WILAYA YA SERENGETI.


Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa NIDA, imeanza kusajili watumishi wa taasisi za Serikali Wilayani Serengeti kwa kutumia mfumo wa kieletroniki kwa lengo la kutoa vitambulisho vya taifa. Aidha zoezi hilo linaenda sambamba na kubaini watumishi hewa pamoja na utambuzi wa vyeti halisi na vya kughushi vya elimu na taaluma.


      Ofisa wa NIDA Fred Mwasipu (kushoto) akiwa anakagua vyeti vya mtumishi mapema jana katika zoezi la uhakiki.

Zoezi hilo litakalofanyika kwa watumishi wa umma wote ndani ya Wilaya ya Serengeti, limefunguliwa na Mkuu wa Wilaya ya Serengeti Nurdin Babu nje ya ofisi yake ambapo watumishi wa umma kutoka taasisi mbali mbali za serikali walihudhuria. "Nashukuru mmefika kufanya kazi hii kubwa hasa katika kipindi hiki ambacho serikali inapambana na watumishi hewa na wenye vyeti feki" alisema Babu, aidha ameiomba NIDA kufanya kazi hiyo kwa weledi na kuhakikisha suala la watumishi hewa linaisha serikalini.

Mheshimiwa Babu amewaagiza watumishi wote wa taasisi za serikali kuhakikisha wanawasilisha nyaraka zote muhimu zinazohitajika kwa zoezi hilo na kufanyiwa usajili na maofisa wa NIDA ndani ya muda wa siku 14 zilizotengwa.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti, Juma Hamsini ambaye naye pia alihudhuria ufunguzi wa zoezi hilo, ameishukuru Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa kwa kufika Serengeti na kufanya zoezi hilo na kuwataka watumishi kutoa ushirikiano na kuondoa hofu iliyokuwepo awali kuhusu shughuli hiyo.

Aidha Msajili Mkuu wa NIDA Wilaya ya Serengeti, Bw. Fred Mwasipu alizitaja changamoto alizozibaini katika hatua ya awali ya ujazaji wa taarifamuhimu katika fomu, ambazo ni; Uwepo watumishi ambao wana vyeti vinavyoonyesha kuwa wamezaliwa Wilaya ya Serengeti ilihali si kweli,Watumishi kubadili majina, kutokuwa na vyeti halisi huku watumishi wengine wakiwa hawana nyaraka muhimu zinazohitajika. Aidha Mwasipu amewaomba watumishi wote kuhakikisha kuwa wanahakikiwa vyeti vyao vyaelimu na taaluma. “Zoezi hili linaenda sambamba na uchukuaji wa taarifa muhimu zitakazotumika katika utengenezaji wa vitambulisho wa taifa”alisema Mwasipu.

Katibu Tawala Wilaya ya Serengeti, Cosmas Qamara alitoa maelezo kuhusu utolewaji na upatikanaji wa vyeti vya kuzaliwa ambapo alisema “Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Serengeti haitoi vyeti vya kuzaliwa kwa mtu yeyote aliyezaliwa nje ya Wilaya ya Serengeti” Qamara amewataka watumishi kuacha kufanya udanganyifu wa mahali pa kuzaliwa na vyema wafike katika ofisi za Wilaya walizozaliwa ili kupata vyeti halisi au kufuata taratibu zilizowekwa na kuwaomba wenye mahitaji kufika katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya kufanya maombi ya kupata vyeti hivyo kulingana na Wilaya walizozaliwa.

Zoezi la usajili wa watumishi wa umma na uhakiki wa nyaraka kwa kutumia mfumo wa kieletroniki, linatarajiwa kuchukua muda wa wiki mbili ambapo maofisa wa NIDA wataweka kambi katika Tarafa 4 ili kuleta ufanisi wa kazi na kuwafikia watumishi wa umma walio mbali na makao makuu ya Wilaya yaliyopo katika Mji wa Mugumu.

                    MATUKIO YALIYOJIRI KATIKA PICHA

  


    Mkuu wa Wilaya ya Serengeti Mhe. Nurdin Babu (kushoto) akihakikiwa na Ofisa wa NIDA.

   Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti, Juma Hamsini (kushoto) akihakikiwa na Ofisa wa NIDA.

   Katibu Tawala Wilaya ya Serengeti  Cosmas Qamar(kushoto) akihakikiwa na Ofisa wa NIDA.

   Watumishi wa Umma wakiwa tayari kwa ajili ya uhakiki.